Matokeo ya utafutaji
Mit 22:24 (SUV)
Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi;
Lk 23:12 (SUV)
Basi siku ile ile Herode na Pilato walipatana kwa urafiki kwa maana hapo kwanza walikuwa na uadui wao kwa wao.
2 Kor 6:14 (SUV)
Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
Mdo 28:7 (SUV)
Karibu na mahali pale palikuwa na mashamba ya mkuu wa kisiwa, jina lake Publio; mtu huyu akatukaribisha kwa moyo wa urafiki, akatufanya wageni wake kwa muda wa siku tatu.
Mdo 12:20 (SUV)
Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni; wakamwendea kwa nia moja, na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha mfalme cha kulalia, wakataka amani; kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya mfalme.
Ayu 29:4 (SUV)
Kama nilivyokuwa katika siku zangu za kukomaa, Hapo siri ya Mungu ilipokuwa hemani mwangu;
2 Pet 1:7 (SUV)
na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo.
Zab 109:4 (SUV)
Badala ya upendo wangu wao hunishitaki, Ijapokuwa naliwaombea.
Zab 109:5 (SUV)
Wamenichukuza mabaya badala ya mema, Na chuki badala ya upendo wangu.
Kum 23:6 (SUV)
Usitafute amani yao wala heri yao siku zako zote, milele.
1 Kor 15:33 (SUV)
Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
1 Sam 18:3 (SUV)
Nao Yonathani na Daudi wakaahidiana, kwa kuwa alimpenda kama roho yake mwenyewe.
Mit 17:9 (SUV)
Afunikaye kosa hutafuta kupendwa; Bali yeye akashifuye neno hutenga rafiki.
Mit 12:26 (SUV)
Mwenye haki ni kiongozi cha mwenzake; Bali njia ya wasio haki huwakosesha.
2 Nya 18:1 (SUV)
Basi, Yehoshafati alikuwa na mali na heshima tele, tena akafanya ujamaa na Ahabu.
Lk 22:48 (SUV)
Yesu akamwambia, Yuda, wamsaliti Mwana wa Adamu kwa kumbusu?
Dan 11:23 (SUV)
Na baada ya maagano atatenda kwa hila; maana atapanda, naye atakuwa hodari pamoja na watu wadogo.
1 Sam 20:42 (SUV)
Naye Yonathani akamwambia Daudi, Enenda kwa amani; kwa maana sisi sote wawili tumeapiana kwa jina la BWANA ya kwamba, BWANA atakuwa kati ya mimi na wewe, na kati ya uzao wangu na uzao wako milele. Daudi akaondoka, akaenda zake; Yonathani naye akaenda zake mjini.
Amo 1:9 (SUV)
Haya ndiyo asemayo BWANA; Kwa makosa matatu ya Tiro, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameitia kabila nzima katika mikono ya Edomu, wala hawakulikumbuka agano la udugu;
Lk 11:8 (SUV)
Nawaambia ya kwamba, ijapokuwa haondoki ampe kwa kuwa ni rafiki yake, lakini kwa vile asivyoacha kumwomba, ataondoka na kumpa kadiri ya haja yake.
Yak 4:4 (SUV)
Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.
Rum 5:10 (SUV)
Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake; zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake.
Ezr 9:12 (SUV)
Basi, msiwape wana wao binti zenu, wala msitwae binti zao kuwa wake za wana wenu, wala msiwatakie amani wala kufanikiwa milele; ili mpate kuwa hodari, na kula wema wa nchi hiyo, na kuwaachia watoto wenu iwe urithi wa milele.
Mit 22:23 (SUV)
Kwa sababu BWANA atawatetea; Naye atawateka uhai wao waliowateka.
Mit 22:25 (SUV)
Usije ukajifunza njia zake; Na kujipatia nafsi yako mtego.