1
Yohane 14:27
BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA
SCLDC10
“Nawaachieni amani; nawapeni amani yangu. Siwapi nyinyi kama vile ulimwengu ufanyavyo. Msiwe na wasiwasi, wala msifadhaike.
Ṣe Àfiwé
Ṣàwárí Yohane 14:27
2
Yohane 14:6
Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai. Hakuna awezaye kwenda kwa Baba ila kwa kupitia kwangu.
Ṣàwárí Yohane 14:6
3
Yohane 14:1
Yesu aliwaambia, “Msifadhaike mioyoni mwenu. Mwaminini Mungu, niaminini na mimi pia.
Ṣàwárí Yohane 14:1
4
Yohane 14:26
lakini Msaidizi, Roho Mtakatifu, ambaye Baba atamtuma kwa jina langu, atawafundisheni kila kitu na kuwakumbusheni yote niliyowaambieni.
Ṣàwárí Yohane 14:26
5
Yohane 14:21
Azipokeaye amri zangu na kuzishika, yeye ndiye anipendaye. Naye anipendaye mimi atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.”
Ṣàwárí Yohane 14:21
6
Yohane 14:16-17
Nami nitamwomba Baba naye atawapeni Msaidizi mwingine, atakayekaa nanyi milele. Yeye ni Roho wa ukweli. Ulimwengu hauwezi kumpokea kwa sababu hauwezi kumwona wala kumjua. Lakini nyinyi mnamjua kwa sababu anabaki nanyi na yu ndani yenu.
Ṣàwárí Yohane 14:16-17
7
Yohane 14:13-14
Na chochote mtakachoomba kwa jina langu nitafanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba chochote kwa jina langu, nitawafanyieni.
Ṣàwárí Yohane 14:13-14
8
Yohane 14:15
“Mkinipenda mtazishika amri zangu.
Ṣàwárí Yohane 14:15
9
Yohane 14:2
Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama isingekuwa hivyo, ningalikwisha waambieni. Sasa nakwenda kuwatayarishieni nafasi.
Ṣàwárí Yohane 14:2
10
Yohane 14:3
Na nikienda na kuwatayarishieni nafasi, nitarudi na kuwachukueni kwangu, ili nanyi muwe pale nilipo mimi.
Ṣàwárí Yohane 14:3
11
Yohane 14:5
Thoma akamwuliza, “Bwana, hatujui unakokwenda, tutawezaje basi, kuijua hiyo njia?”
Ṣàwárí Yohane 14:5