1
2 Wathesalonike 2:3
Neno: Bibilia Takatifu
Mtu yeyote na asiwadanganye kwa namna yoyote kwa maana siku ile haitakuja mpaka uasi utokee kwanza, na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa.
Linganisha
Chunguza 2 Wathesalonike 2:3
2
2 Wathesalonike 2:13
Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho kwa kuiamini kweli.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:13
3
2 Wathesalonike 2:4
Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:4
4
2 Wathesalonike 2:16-17
Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, awafariji mioyo yenu na kuwaimarisha katika kila neno na tendo jema.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:16-17
5
2 Wathesalonike 2:11
Kwa sababu hii, Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu, ili waendelee kuamini uongo
Chunguza 2 Wathesalonike 2:11
6
2 Wathesalonike 2:9-10
Kuja kwa yule mwasi kutaonekana kana kwamba ni kutenda kazi kwake Shetani ambaye hutumia nguvu zote, ishara, maajabu ya uongo, na kila aina ya uovu kwa wale wanaoangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:9-10
7
2 Wathesalonike 2:7
Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:7
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video