1
1 Wathesalonike 5:16-18
Swahili Revised Union Version
Furahini siku zote; ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.
Linganisha
Chunguza 1 Wathesalonike 5:16-18
2
1 Wathesalonike 5:23-24
Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe muwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo. Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:23-24
3
1 Wathesalonike 5:15
Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:15
4
1 Wathesalonike 5:11
Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, hakika kama mnavyofanya.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:11
5
1 Wathesalonike 5:14
Ndugu, tunawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:14
6
1 Wathesalonike 5:9
Kwa kuwa Mungu hakutuweka ili tupate hasira yake, bali ili tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo
Chunguza 1 Wathesalonike 5:9
7
1 Wathesalonike 5:5
Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:5
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video