Nami nitawapeleka katika hiyo nchi, niliyoiapia na kuuinua mkono wangu kwamba: Nitampa Aburahamu na Isaka na Yakobo; hiyo ndiyo, mimi Bwana nitakayowapa ninyi, iwe yenu. Mose alipowaambia wana wa Isiraeli maneno haya, hawakumsikia Mose, kwa kuwa roho zao zilikuwa zimesongeka, kazi zikizidi kuwa ngumu.