1
Mhubiri 3:1
Biblia Habari Njema
Kila kitu kina majira yake, kila jambo duniani lina wakati wake
Linganisha
Chunguza Mhubiri 3:1
2
Mhubiri 3:2-3
Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa; wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa; wakati wa kuua na wakati wa kuponya; wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga
Chunguza Mhubiri 3:2-3
3
Mhubiri 3:4-5
wakati wa kulia na wakati wa kucheka; wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza; wakati wa kutupa mawe na wakati wa kuyakusanya mawe pamoja; wakati wa kukumbatia na wakati wa kuacha kukumbatia
Chunguza Mhubiri 3:4-5
4
Mhubiri 3:7-8
wakati wa kurarua na wakati wa kushona; wakati wa kukaa kimya na wakati wa kuongea; wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia; wakati wa vita na wakati wa amani.
Chunguza Mhubiri 3:7-8
5
Mhubiri 3:6
wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza; wakati wa kuhifadhi na wakati wa kutupa
Chunguza Mhubiri 3:6
6
Mhubiri 3:14
Najua kwamba lolote atendalo Mungu linadumu milele. Hakuna kinachoweza kuongezwa wala kupunguzwa; Mungu amefanya mambo yawe hivyo kusudi wanadamu wamche yeye.
Chunguza Mhubiri 3:14
7
Mhubiri 3:17
Basi, nikasema moyoni mwangu, “Haidhuru! Mungu atawahukumu waadilifu, hali kadhalika na waovu, maana amepanga wakati maalumu kwa kila jambo na kwa kila kazi.”
Chunguza Mhubiri 3:17
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video