1
Mhubiri 5:2
Biblia Habari Njema
Fikiri kabla ya kusema, wala usiwe mwepesi kusema chochote mbele ya Mungu, kwa maana Mungu yuko mbinguni na wewe uko duniani. Kwa hiyo usiseme mengi.
Linganisha
Chunguza Mhubiri 5:2
2
Mhubiri 5:19
Kama Mungu anampa mtu utajiri na mali na kumjalia fursa ya kufurahia hayo, basi binadamu ashukuru na avifaidi hivyo alivyojipatia kwa jasho lake. Hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Chunguza Mhubiri 5:19
3
Mhubiri 5:10
Apendaye fedha hatatosheka na fedha; wala atamaniye mali hata akiipata hatatosheka. Hilo nalo ni bure kabisa.
Chunguza Mhubiri 5:10
4
Mhubiri 5:1
Uwe mwangalifu uendapo katika nyumba ya Mungu, na kukaribia ili kusikiliza kwa makini kuliko kutambika kama watambikavyo wapumbavu, watu wasiopambanua kati ya jema na ovu.
Chunguza Mhubiri 5:1
5
Mhubiri 5:4
Ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuitimiza; na Mungu hapendezwi na wapumbavu. Tekeleza ulichoahidi.
Chunguza Mhubiri 5:4
6
Mhubiri 5:5
Ni afadhali kutoweka nadhiri kuliko kuweka nadhiri kisha usiitimize.
Chunguza Mhubiri 5:5
7
Mhubiri 5:12
Usingizi wa kibarua ni mtamu, awe ameshiba au amekula kidogo tu. Lakini usingizi wa tajiri ni wa wasiwasi daima, maana ziada ya mali yake humsumbua usiku kucha.
Chunguza Mhubiri 5:12
8
Mhubiri 5:15
Kama vile binadamu alivyokuja duniani uchi toka tumboni mwa mama yake, ndivyo atakavyorudi uchi huko alikotoka. Hataweza kuchukua hata sehemu ndogo ya mapato ya kazi yake.
Chunguza Mhubiri 5:15
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video