Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Timotheo 5:17-20

1 Timotheo 5:17-20 NENO

Wazee wa kundi la waumini wanaoongoza shughuli za kundi hilo vizuri wanastahili heshima mara mbili, hasa wale ambao kazi yao ni kuhubiri na kufundisha. Kwa maana Maandiko husema, “Usimfunge maksai kinywa apurapo nafaka,” tena, “Mfanyakazi anastahili mshahara wake.” Usiendekeze mashtaka dhidi ya mzee isipokuwa yawe yameletwa na mashahidi wawili au watatu. Wale wanaodumu katika dhambi uwakemee hadharani, ili wengine wapate kuogopa.