Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Timotheo 5:17-20

1 Timotheo 5:17-20 BHN

Viongozi wa kanisa wanaowaongoza watu vizuri wanastahili kupata riziki maradufu, hasa wale wanaofanya bidii katika kuhubiri na kufundisha. Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Usimfunge ng'ombe kinywa anapopura nafaka,” na tena “Mfanyakazi astahili malipo yake.” Usikubali kupokea mashtaka dhidi ya mzee yasipowakilishwa na mashahidi wawili au watatu. Wale wanaotenda dhambi waonye hadharani, ili wengine wapate kuogopa.