Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Amosi 3

3
Mashahidi waitwa dhidi ya Israeli
1Sikilizeni neno hili alilosema Mwenyezi Mungu dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:
2“Ni ninyi tu niliowachagua
kati ya jamaa zote za dunia;
kwa hiyo nitawaadhibu
kwa ajili ya dhambi zenu zote.”
3Je, watu wawili hutembea pamoja
wasipokubaliana kufanya hivyo?
4Je, simba hunguruma katika kichaka
wakati hana mawindo?
Aweza kuvuma katika pango
wakati ambao hajakamata chochote?
5Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini
ambapo hajategewa chambo?
Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini
wakati hakuna chochote cha kunasa?
6Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari,
watu hawatetemeki?
Mji unapopatwa na maafa,
je, si Mwenyezi Mungu amesababisha?
7Hakika Bwana Mungu Mwenyezi hatafanya neno lolote
bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
8Simba amenguruma:
je, ni nani ambaye hataogopa?
Bwana Mungu Mwenyezi ametamka:
je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?
9Tangazeni katika ngome za Ashdodi
na katika ngome za Misri:
“Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria;
angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake,
na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”
10Mwenyezi Mungu asema: “Hawajui kutenda lililo jema,
wale ambao hujilundikia nyara
na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”
11Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi:
“Adui ataizingira nchi;
ataangusha chini ngome zenu
na kuteka nyara maboma yenu.”
12Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu:
“Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba
vipande viwili tu vya mfupa wa mguu
au kipande cha sikio,
hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa,
wale wanaokaa Samaria
kwenye kingo za vitanda vyao,
na katika Dameski
kwenye viti vyao vya fahari.”
13“Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, yeye Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni.
14“Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake,
nitaharibu madhabahu za Betheli;
pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali
na kuanguka chini.
15Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika,
pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi;
nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu
na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,”
asema Mwenyezi Mungu.

Iliyochaguliwa sasa

Amosi 3: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia