Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kutoka 25:31-40

Kutoka 25:31-40 NENO

“Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja. Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine. Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa. Juu ya kinara chenyewe vitakuwa vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi, yakiwa na matovu yake na maua yake. Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla. Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi. “Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake. Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi. Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote. Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano uliooneshwa kule mlimani.