Hosea Utangulizi
Utangulizi
Hosea mwana wa Beeri alikuwa mzaliwa wa Ufalme wa Kaskazini, yaani Israeli, ambao pia uliitwa Efraimu. Maana ya jina Hosea ni “Wokovu”. Huduma ya Hosea kwa Ufalme wa Kaskazini ilikaribiana sana na ile ya Amosi. Hawa wawili ndio manabii pekee wa vitabu vya Manabii ambao vitabu vyao vilihusu Ufalme wa Kaskazini na maangamizi yake.
Hosea alianza huduma yake miaka ya baadaye ya utawala wa Yeroboamu wa Pili, wakati Israeli ikifurahia utulivu wa kisiasa na ustawi wa kiuchumi. Kufuatia kifo cha Yeroboamu wa Pili mnamo 753 K.K., hali ya taifa la Israeli ilibadilika. Amani na utulivu katika taifa vilitoweka. Taifa likaporomoka na kuangamia. Waisraeli wakapigwa na Waashuru na kisha kupelekwa uhamishoni mnamo 722 K.K.
Mwandishi
Hosea.
Kusudi
Kuonesha upendo mkuu wa Mwenyezi Mungu kwa Waisraeli waliokuwa wamemwasi. Watu wanapomwacha na kumwasi, Mwenyezi Mungu anaendelea kuwapenda na kuwarejesha kwake.
Mahali
Ufalme wa Kaskazini yaani Israeli, ambao uliitwa Efraimu.
Tarehe
Mnamo 715–710 K.K.
Wahusika Wakuu
Hosea, Gomeri, na watoto wao.
Wazo Kuu
Hukumu na upendo mkuu wa Mwenyezi Mungu kwa watu wake.
Mambo Muhimu
Hosea anaelezea hali ya taifa la Israeli akitumia hali iliyojitokeza katika maisha ya kila siku. Mwenyezi Mungu anafananishwa na: mume, baba, simba, chui, dubu, umande, mvua, nondo, na mifano mingine. Israeli inafananishwa na: mke aliyekosa uaminifu kwa mumewe, mtu mgonjwa, mzabibu, mzeituni, mwanamke anayejifungua, jiko la kuokea, ukungu wa asubuhi, makapi, moshi, na mifano mingine.
Yaliyomo
Maisha ya Hosea katika jamii (1:1–3:5)
Hali ya dhambi ya Israeli (4:1–10:15)
Hukumu ya Mwenyezi Mungu na rehema zake (11:1–14:9).
Iliyochaguliwa sasa
Hosea Utangulizi: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
![None](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapistaging.com%2F58%2Fhttps%3A%2F%2Fweb-assets.youversion.com%2Fapp-icons%2Fsw.png&w=128&q=75)
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.