Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayubu 38:25-38

Ayubu 38:25-38 NEN

Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi, ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake, ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake? Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande? Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni, wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda? “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni? Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake? Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani? “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji? Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’? Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu? Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Ayubu 38:25-38