Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayu 38:25-38

Ayu 38:25-38 SUV

Ni nani aliyepasua mfereji kwa maji ya gharika, Au njia kwa umeme wa radi; Kunyesha mvua juu ya nchi isiyo na watu; Juu ya jangwa asiyokaa mwanadamu; Kuishibisha nchi iliyo kame na ukiwa, Na kuyameza majani yaliyo mororo? Je! Mvua ina baba? Au ni nani aliyeyazaa matone ya umande? Barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na sakitu ya mbinguni ni nani aliyeizaa? Maji hugandamana kama jiwe, Na uso wa vilindi huganda kwa baridi. Je! Waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia, Au kuvilegeza vifungo vya Orioni? Je! Waweza kuziongoza Sayari kwa wakati wake? Au waweza kuongoza Dubu na watoto wake? Je! Unazijua amri zilizoamuriwa mbingu? Waweza kuyathibitisha mamlaka yake juu ya dunia? Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, ili wingi wa maji ukufunikize? Waweza kuutuma umeme, nao ukaenda, Ukakuambia, Sisi tupo hapa? Je! Ni nani aliyetia hekima moyoni? Au ni nani aliyetia ufahamu rohoni? Ni nani awezaye kuyahesabu mawingu kwa hekima? Au ni nani awezaye kuzimimina chupa za mbinguni? Wakati mavumbi yagandamanapo, Na madongoa kushikamana pamoja?

Soma Ayu 38

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Ayu 38:25-38