Mithali 24:7-12
Mithali 24:7-12 NENO
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema. Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila. Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka. Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo! Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni. Mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?