Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kutoka 25:1-9

Kutoka 25:1-9 BHN

Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli wanipe michango ya matoleo, nawe upokee kwa niaba yangu. Utapokea kutoka kwa mtu yeyote atakayetoa kwa moyo mkunjufu. Utapokea matoleo yafuatayo: Dhahabu, fedha, shaba, sufu ya buluu, ya zambarau na nyekundu, kitani safi iliyosokotwa manyoya ya mbuzi; ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, ngozi za mbuzi, mbao za mjohoro, mafuta kwa ajili ya taa, viungo kwa ajili ya mafuta ya kuweka wakfu na kwa ajili ya ubani wenye harufu nzuri, vito vya sardoniki, na vito vingine kwa ajili ya mapambo ya kizibao cha kuhani na kifuko cha kifuani. Vilevile Waisraeli watanitengenezea hema takatifu, ili niweze kukaa kati yao. Utatengeneza hema hiyo na vifaa vyake kulingana na mfano nitakaokuonesha.

Soma Kutoka 25