Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yobu 38:25-38

Yobu 38:25-38 BHN

“Nani aliyechora angani njia kwa ajili ya mvua? Nani aliyeionesha radi njia yake mawinguni, ikasababisha mvua kunyesha nchini kusikoishi mtu na jangwani ambako hakuna mtu, ili kuiburudisha nchi kavu na kame na kuifanya iote nyasi? “Je, mvua ina baba? Au nani ameyazaa matone ya umande? Je, barafu ilitoka tumboni kwa nani? Nani aliyeizaa theluji? Maji hugeuka kuwa magumu kama jiwe, na uso wa bahari ukaganda. “Angalia makundi ya nyota: Je, unaweza kuifunga minyororo Kilimia, au kuvilegeza vifungo vya Orioni? Je, waweza kuziongoza nyota katika majira yake, au kumwongoza Dubu pamoja na watoto wake? Je, wazijua kanuni zinazotawala mbingu; Je, waweza kuzipangia taratibu zao duniani? “Je, waweza kupaza sauti na kuyaamuru mawingu yakufunike kwa mtiririko wa mvua? Je, wewe ukiamuru umeme umulike, utakujia na kusema: ‘Nipo hapa?’ Ni nani aliyemjulisha kwarara kujaa kwa mto Nili au aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja? Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu, au kuinamisha viriba vya maji huko mbinguni? ili vumbi duniani igandamane na udongo ushikamane na kuwa matope?

Soma Yobu 38

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Yobu 38:25-38