Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 136

136
Wimbo wa shukrani
1 # Taz Zab 100:5; 106:1; 107:1; 118:1 Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
2Mshukuruni Mungu wa miungu;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
3Mshukuruni Bwana wa mabwana;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
4Ndiye peke yake atendaye makuu ya ajabu;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
5Ndiye aliyeziumba mbingu kwa hekima;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
6Ndiye aliyeitengeneza nchi juu ya vilindi vya maji;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
7Ndiye aliyeumba jua, mwezi na nyota;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
8Jua liutawale mchana;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
9Mwezi na nyota vitawale usiku;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
10Ndiye aliyewaua wazaliwa wa kwanza wa Misri;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
11Akawaondoa watu wa Israeli kutoka huko;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
12Kwa mkono wake wenye nguvu na enzi;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
13Ndiye aliyeigawa Bahari ya Shamu sehemu mbili;
kwa maana fadhili zake zadumu milele,
14akawapitisha watu wa Israeli humo;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
15Lakini akawazamisha humo Farao na jeshi lake;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
16Ndiye aliyewaongoza watu wake jangwani;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
17Ndiye aliyewapiga wafalme wenye nguvu;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
18Akawaua wafalme maarufu;
kwa maana fadhili zake zadumu milele;
19akamuua Sihoni, mfalme wa Waamori,
kwa maana fadhili zake zadumu milele;
20na Ogu, mfalme wa Bashani;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
21Akachukua nchi zao akawapa watu wake;
kwa maana fadhili zake zadumu milele;
22ziwe riziki ya Israeli, mtumishi wake;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
23Ndiye aliyetukumbuka wakati wa unyonge wetu;
kwa maana fadhili zake zadumu milele;
24akatuokoa kutoka maadui zetu;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
25Ndiye akipaye kila kiumbe chenye uhai chakula;
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
26Mshukuruni Mungu wa mbinguni;
kwa maana fadhili zake zadumu milele!

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 136: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia