Zaburi 45:9-17
Zaburi 45:9-17 Biblia Habari Njema (BHN)
Binti za wafalme ni baadhi ya wanaokulaki, naye malkia amesimama kulia kwako, amevaa mapambo ya dhahabu safi ya Ofiri. Sikiliza binti, ufikirie! Tega sikio lako: Sahau sasa watu wako na jamaa zako. Uzuri wako wamvutia mfalme; yeye ni bwana wako, lazima umtii. Watu wa Tiro watakuletea zawadi; matajiri watataka upendeleo wako. Binti mfalme anaingia mzuri kabisa! Vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu. Akiwa amevalia vazi la rangi nyingi, anaongozwa kwa mfalme, akisindikizwa na wasichana wenzake; nao pia wanapelekwa kwa mfalme. Kwa furaha na shangwe wanafika huko, na kuingia katika jumba la mfalme. Ee mfalme, utapata watoto wengi watakaotawala mahali pa wazee wako; utawafanya watawale duniani kote. Nitalifanya jina lako litukuzwe katika vizazi vyote, nayo mataifa yatakusifu daima na milele.
Zaburi 45:9-17 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Binti za wafalme wamo Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Katika mkono wako wa kulia amesimama malkia Akiwa amevaa dhahabu safi ya Ofiri. Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. Naye mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie. Na watu wa Tiro wanakushawishi kwa zawadi, Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako. Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu. Anapelekwa kwa mfalme Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. Wanawali wenzake wanaomfuata, Pia watapelekwa kwako. Watapelekwa kwa furaha na shangwe, Na kuingia katika nyumba ya mfalme. Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote. Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu Katika vizazi vyote. Kwa hiyo mataifa watakushukuru Milele na milele.
Zaburi 45:9-17 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Binti za wafalme wamo Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Mkono wako wa kuume amesimama malkia Amevaa dhahabu ya Ofiri. Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. Naye mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie. Na binti Tiro analeta kipawa chake, Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako. Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu. Atapelekwa kwa mfalme Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. Wanawali wenzake wanaomfuata, Watapelekwa kwako. Watapelekwa kwa furaha na shangwe, Na kuingia katika nyumba ya mfalme. Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote. Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu Katika vizazi vyote. Kwa hiyo mataifa watakushukuru Milele na milele.
Zaburi 45:9-17 Neno: Maandiko Matakatifu 2024 (NENO)
Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri. Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako. Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako. Binti Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako. Ufahari wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu. Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako. Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme. Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote. Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.