Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 5Mfano

Soma Biblia Kila Siku 5

SIKU 14 YA 31

Danieli alikuwa katika wakati mgumu. Ndoto ya mfalme isipoelezwa na kutafsiriwa, matokeo yake yatakuwa ni kuuawa yeye, rafikize na wengine wa Babeli. Mtumishi wa Mungu, Danieli, anawashirikisha rafikize ili waingie katika maombi. Bila rehema ya Mungu haitawezekana. Mungu hujibu maombi, na kufunua siri ile. Ufunuo huo haumpi Danieli kiburi cha kujisifia kuwa anaweza. Kinachomlinda ni kwamba anamrudishia Mungu sifa zote. Tumia m.20-23 katika maombi yako ukimshukuru Mungu kwa aliyokupa.

siku 13siku 15

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 5

Soma Biblia Kila Siku 5 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz/