Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Tafakari Kuhusu HakiMfano

Tafakari Kuhusu Haki

SIKU 4 YA 31

Nikiwa hivi karibuni nimetembelea mlima wa kuvutia huko Banff, Alberta, ilikuwa rahisi kwa nafsi na moyo wangu kupaza sauti za kumsifu Mungu, Muumba wetu, nilipokaa kwa kuvutiwa juu ya mlima. Kwa kweli ulikuwa wakati wa aina yake! Ni muhimu sifa za aina hii zitafsiriwe katika maisha yetu ya kila siku.

Mwandishi Ann Voskamp anaandika, ‘Tulilazimika kuishi kwa mkao wa kuabudu kwa shukurani, na tunapoishi kwa sifa tunaliishi kusudi letu, na vipande vyote huanguka mahali pake, sisi sote tukianguka chini kwa shukrani.’

Tunapotengeneza mkao wa shukurani kila siku katika dunia iliyojaa vurugu, utafurika katika shuhuda zetu. Moja ya nyimbo zangu pendwa za kuabudu ni ‘Namzungumza Yesu’. Mstari mmoja unajitokeza ndani yangu: ‘Paza sauti Yesu kutoka milimani, Yesu mitaani...’ Hebu kila mara tuwe na hamu ya kutangaza sifa zake!

Changamoto: Tunawezaje kufanya sifa ziwe mtindo wa maisha? Kila siku utamsifu, kila siku utawashirikisha wengine Yesu ni nani na kila siku utazungumza juu ya jina lenye nguvu la Yesu.

Maombi: Bwana, naomba sifa zangu kwako zipazwe na ziwe thabiti, zitangaze wewe kuwa ndiye mtakatifu na mwenye haki, uletaye furaha na amani nafsini mwetu.

siku 3siku 5

Kuhusu Mpango huu

Tafakari Kuhusu Haki

Mfululizo wa tafakari ya kila siku kuhusu haki, ulioandikwa na wanawake kutoka kote katika dunia ya Jeshi la Wokovu. Maswala ya haki ya jamii yako mbele sana ya mawazo yetu siku hizi. Mkusanyo huu wa tafakari kuhusu haki ya jamii umeandikwa na wanawake kutoka kote duniani wenye nia na hamu ya kuwasaidia wengine katika jina la Kristo.

More

Tungependa kumshukuru The Salvation Army International kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://salvationarmy.org