YouVersion Logo
Search Icon

Matendo ya Mitume 10

10
Habari ya Petro na Kornelio
1Katika muji Kaisaria, kulikuwa mutu mumoja jina lake Kornelio. Yeye alikuwa mukubwa wa kundi la waaskari lililoitwa “Kundi la Italia.” 2Yeye alikuwa mwenye kuogopa Mungu, naye alimwabudu Mungu pamoja na watu wote waliokuwa kwake. Aliwasaidia wamasikini wengi, naye alikuwa akimwomba Mungu siku zote. 3Siku moja, ilipokuwa saa tisa ya muchana, akaona maono. Aliona waziwazi malaika wa Mungu akiingia kwake na kumwambia: “Kornelio!”
4Kornelio akamukazia macho akiwa ameshikwa na woga, akamwuliza: “Bwana, ni nini?”
Malaika akamujibu: “Mungu amesikia maombi yako na kupendezwa na misaada unayotoa kwa wamasikini, na kwa hiyo anakukumbuka. 5Basi sasa; uwatume watu Yopa waende kumwita mutu mumoja jina lake Simoni anayeitwa vilevile Petro. 6Anapanga kwa fundi mumoja wa kutengeneza vitu vya ngozi, anayeitwa Simoni. Nyumba yake iko pembeni ya bahari.”
7Yule malaika aliyesema na Kornelio alipoondoka, akawaita watu wawili kati ya watumishi wake na askari mumoja mwenye kuogopa Mungu, aliyekuwa mumoja wa wasimamizi wake wa kipekee. 8Na kisha kuwaelezea mambo yote yaliyotokea, akawatuma Yopa.
9Kesho yake karibu na saa sita ya muchana, hao watu watatu wakafika karibu na Yopa, saa ile Petro akapanda juu ya paa kwa kuomba. 10Naye akasikia njaa, na kuhitaji chakula. Walipokuwa wakimutengenezea chakula, akakuwa sawa amezimia. 11Akaona katika maono mbingu imefunguliwa wazi, na kitu kimoja kinachokuwa kama nguo kubwa kikishuka, kikitelemushwa mpaka chini, kikishikwa kwenye pembe zake ine. 12Na ndani yake kulikuwa kila namna ya nyama wenye miguu mine na wenye kutambaa pamoja na ndege. 13Kisha akasikia sauti ikimwambia: “Petro, simama. Chinja na ukule!”
14Lakini Petro akajibu: “Hapana, hata kidogo Ee Bwana! Mimi sijakula bado kitu chochote kisichoruhusiwa kukuliwa, wala chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu.”
15Lakini ile sauti ikamurudilia, ikisema: “Vitu vilivyotakaswa na Mungu, usivihesabu kuwa vichafu.”
16Nayo maneno haya yakasikilika tena mara tatu, kisha chombo kile kikanyanyuliwa mbinguni.
17Petro alipokuwa angali na wasiwasi, naye akijiuliza juu ya maana ya maono yale, wale watu waliotumwa na Kornelio wakafika mbele ya mulango kwa maana walikuwa wamekwisha kujulishwa nafasi gani kunapokuwa nyumba ya Simoni. 18Wakapiga hodi wakiuliza kama Simoni anayeitwa vilevile Petro anapanga pale.
19Petro akiwa akifikiri juu ya maana ya yale maono, Roho Mutakatifu akamwambia: “Kuna watu watatu hapa wanaokutafuta. 20Basi, simama ushuke na kwenda pamoja nao pasipo kusita, kwa maana ni mimi niliyewatuma.”
21Halafu Petro akashuka na kuwaambia wale watu: “Ni mimi munayemutafuta. Mumekuja hapa kwa sababu gani?”
22Nao wakamujibu: “Tumetumwa hapa na Kornelio, mukubwa wa waaskari. Yeye ni mutu wa haki na mwenye kumutii Mungu, naye anasifiwa na Wayuda wote. Malaika mutakatifu amemutokea na kumwagiza akuite ufike kwake kusudi asikie maneno utakayomwambia.”
23Kisha Petro akawakaribisha ndani ya nyumba na kuwapangisha mule.
Kesho yake Petro akafunga safari pamoja nao. Na wandugu waamini wamoja waliokaa Yopa wakamusindikiza. 24Kesho kutwa wakafika katika muji Kaisaria. Kornelio alikuwa akiwangojea pamoja na jamaa yake na warafiki zake aliowaalika. 25Petro alipokuwa akiingia ndani ya nyumba, Kornelio akaenda kumupokea, akapiga magoti mbele yake na kumwabudu. 26Lakini Petro akamwinua Kornelio na kumwambia: “Simama, kwa maana mimi ni mutu kama wewe.”
27Petro akaingia ndani ya nyumba akiwa akisimulia na Kornelio, na mule akakuta watu wengi wamekusanyika. 28Akawaambia: “Ninyi munajua wazi kama katika Sheria ya dini yetu inakatazwa kwa Muyuda kushirikiana na mutu wa taifa lingine wala kumutembelea. Lakini Mungu amenionyesha kwamba haifai kumuhesabia mutu yeyote kuwa muchafu wala mutengwa. 29Ni kwa sababu hii, wakati uliponitumia wajumbe, nilikuja pasipo kusita. Basi sasa ningependa kujua kwa sababu gani muliniita.”
30Kornelio akajibu: “Kumekwisha kupita siku tatu, mimi nilikuwa nikiomba ndani ya nyumba yangu kwa saa hii hii ya saa tisa ya muchana. Mara moja nikaona mutu anayevaa nguo yenye kungaa sana, akisimama mbele yangu. 31Naye akaniambia: ‘Kornelio, Mungu amesikia maombi yako na kukukumbuka kwa ajili ya misaada unayotoa kwa wamasikini. 32Basi tuma watu waende Yopa kwa kumwita mutu mumoja jina lake Simoni anayeitwa vilevile Petro. Naye anapanga kwa fundi mumoja anayetengeneza vitu vya ngozi anayeitwa Simoni. Nyumba yake iko pembeni ya bahari.’ 33Na pale pale nikatuma watu kwako, nawe umefanya vizuri kwa kufika. Sasa sisi wote tuko hapa mbele ya Mungu kwa kusikiliza mambo yote Bwana aliyokuagiza kutuambia.”
Hotuba ya Petro
34Basi Petro akaanza kuhubiri, akisema: “Sasa ninafahamu kwamba Mungu hana upendeleo, 35lakini katika kila taifa mutu yeyote anayemutii Mungu na kutenda yanayokuwa ya haki, anamupendeza. 36Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote. 37Ninyi munajua mambo yaliyotokea katika Yudea yote, yakianzia katika jimbo la Galilaya nyuma ya mahubiri ya Yoane yaliyoelekea ubatizo. 38Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye. 39Na sisi tuko washuhuda wa mambo yote Yesu aliyofanya katika inchi ya Wayuda na katika muji wa Yerusalema. Walimwua kwa kumutundika juu ya musalaba, 40lakini Mungu akamufufua kwa siku ya tatu kisha kufa kwake na kumwonyesha waziwazi. 41Hakuonekana kwa watu wote, lakini kwa sisi tuliochaguliwa na Mungu kuwa washuhuda. Ni sisi tuliokula na kunywa pamoja naye nyuma ya kufufuka kwake. 42Akatuagiza kutangaza Habari Njema kwa watu na kushuhudia kwamba ni yeye aliyewekwa na Mungu kuwa Mwamuzi wa wazima na wafu. 43Manabii wote wanamushuhudia Yesu kwamba kila mutu anayemwamini atasamehewa zambi zake kwa uwezo wa jina lake.”
Watu wamoja wa mataifa mengine wanapokea Roho Mutakatifu
44Petro alipokuwa hajamaliza kusema maneno hayo, Roho Mutakatifu akashuka juu ya wote waliosikiliza mahubiri yake. 45Na wale wanafunzi Wayuda waliofika pamoja na Petro wakashangaa sana kwa kuona kwamba Mungu ametoa zawadi ya Roho wake Mutakatifu kwa watu wa mataifa mengine vilevile. 46Kwa maana waliwasikia wakisema kwa luga za ajabu na kumutukuza Mungu. Halafu Petro akasema: 47“Ni nani anayeweza kuwazuiza watu hawa waliopewa Roho Mutakatifu kama sisi wasibatizwe kwa maji?”
48Basi akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Na kisha wakamusihi Petro akae kule kwao kwa siku chache.

Currently Selected:

Matendo ya Mitume 10: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

Video for Matendo ya Mitume 10