1
Hes 21:8
Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia
Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi.
Linganisha
Chunguza Hes 21:8
2
Hes 21:9
Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi.
Chunguza Hes 21:9
3
Hes 21:5
Watu wakamnung’unikia Mungu, na Musa, Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misri, ili tufe jangwani? Maana hapana chakula, wala hapana maji, na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu.
Chunguza Hes 21:5
4
Hes 21:6
BWANA akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa.
Chunguza Hes 21:6
5
Hes 21:7
Watu wakamwendea Musa, wakasema, Tumefanya dhambi kwa sababu tumemnung’unikia Mungu, na wewe; utuombee kwa BWANA, atuondolee nyoka hawa. Basi Musa akawaombea watu.
Chunguza Hes 21:7
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video