Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Obadia 1:1-14

Obadia 1:1-14 NENO

Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Mwenyezi Mungu: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.” “Tazama, nitakufanya mdogo miongoni mwa mataifa, utadharauliwa kabisa. Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika mapango ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’ Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Mwenyezi Mungu. “Ikiwa wezi wangekuja kwako, ikiwa wanyang’anyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache? Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara! Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua. “Katika siku hiyo,” asema Mwenyezi Mungu, “je, sitaangamiza wenye hekima wa Edomu, hao wenye ufahamu katika milima ya Esau? Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa. Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele. Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake, na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao. Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao. Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyang’anya mali yao katika siku ya maafa yao. Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.