Zaburi 36:5-7
Zaburi 36:5-7 NEN
Upendo wako, Ee BWANA, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga. Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee BWANA, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama. Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.