Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mit 25:18-28

Mit 25:18-28 SUV

Mtu amshuhudiaye jirani yake uongo Ni nyundo, na upanga, na mshale mkali. Kumtumaini asiye mwaminifu wakati wa taabu Ni kama jino lililovunjika, au mguu ulioteguka. Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito, Ni kama yeye avuaye nguo wakati wa baridi; Ni kama siki juu ya magadi. Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa; Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na BWANA atakupa thawabu. Upepo wa kusi huleta mvua; Vile vile asingiziaye huleta uso wa ghadhabu. Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi. Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu, Ndivyo ilivyo habari njema itokayo katika nchi ya mbali. Mwenye haki amwangukiapo mtu mbaya Ni kama chemchemi iliyochafuka, Na kisima kilichokanyagwa. Haifai kula asali nyingi mno; Vile vile mtu kutafuta utukufu wake mwenyewe si utukufu. Asiyetawala roho yake Ni mfano wa mji uliobomolewa, usio na kuta.

Soma Mit 25

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Mit 25:18-28