Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 03/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 03/2024

SIKU 7 YA 31

Mungu hutumia wajumbe akitengeneza nyumba yake hapa duniani, yaani watu wake. Katika agano la kale mjumbe alikuwa ni Musa, katika agano jipya ni Yesu. Wote wawili walithibitika kuwa waaminifu katika kazi yao. Lakini Yesu ana heshima zaidi ya Musa, kama kazi yake ilivyo na maana zaidi. Wakati Musa alikuwa ni mtumishi tu, Yesu ni Mwana wa Mungu. Kwa hiyo tumzingatie sana Yesu. Yeye ndiye fahari na tumaini la nyumba takatifu ya Mungu ambamo sisi tumo kama tukishikamana naye kwa imani mpaka mwisho.

Andiko

siku 6siku 8

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 03/2024

Soma Biblia Kila Siku 03/ 2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Waebrania. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/