Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 03/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 03/2024

SIKU 31 YA 31

Yesu alipokufa, wanafunzi wake waliishi kwa mashaka na hofu ya kuwaogopa Wayahudi. Lakini kufufuka kwa Yesu Jumapili ya Pasaka kuliwaletea tumaini la maisha mapya kimwili na kiroho. Sisi tunamhubiri Yesu kuwa amefufuka na yu hai. Kama alivyojifunua kwa wanafunzi, leo yupo kwetu kutuokoa na kutusamehe dhambi zetu. Pia kufufuka kwake kunatuhakikishia ndiye Mwana wa Mungu, na kunatupa tumaini la kufufuka siku ya mwisho. Umkaribishe Yesu aliyefufuka moyoni mwako ili ashughulike na maisha yako nawe utaona baraka zake.

siku 30

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 03/2024

Soma Biblia Kila Siku 03/ 2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Waebrania. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/