Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 03/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 03/2024

SIKU 24 YA 31

Leo ni siku ya Mitende. Baada ya siku chache Yesu atasulubishwa, Yohana anasimulia vizuri matayarisho ya kifo cha Yesu. Pilato hakuona kosa la Yesu, lakini alimwacha mikononi mwa Wayahudi wamsulubishe ili kumheshimu Kaisari na ili kutunza mahusiano na Wayahudi. Ni vema kutenda kweli ili kuwa na mahusiano mazuri na Mungu badala ya wanadamu. Pia ni vema kujua Yesu aliteswa na kuuawa kwa ajili ya dhambi zetu ili atuokoe. Tuepuke kutenda dhambi ili tusimsulubishe Yesu mara ya pili, kwani yeyeni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso(Zab 46:1).

siku 23siku 25

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 03/2024

Soma Biblia Kila Siku 03/ 2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Waebrania. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/