Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 04/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 04/2025

SIKU 16 YA 30

Musa anatoa mwongozo kwa Haruni na wanawe waliobaki wasije wakakosea na wao wakafa. Watunze utakatifu wa kimungu ili watu wa Israeli wasiangamizwe. Kwa hiyo hawapewi ruhusa ya kushughulikia mazishi ya ndugu zao. Vilevile wasitumie kileo chochote wakati wa kufanya kazi ya Mungu, isije ikatokea tena kufanya kinyume na maagizo yake. Badala yake tunashauriwa kujazwa Roho.Msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho(Efe 5:18). Tukiendelea kusoma mistari inayofuata (Efe 5:19-21) tunajifunza jinsi inavyowezekana kujazwa hivyo.Mjazwe Roho, mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo; hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo. Mapenzi ya Mungu hutimizwa tukimtanguliza yeye kwa kila jambo.

siku 15siku 17

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 04/2025

Soma Biblia Kila Siku 04/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Aprili pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Walawi, Luka na 2 Petro. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz