Soma Biblia Kila Siku 07/2025Mfano

Bonde la maono ni jiji la Yerusalemu. Hapa ni mahali Mungu alipojifunua mwenyewe kwa ajili ya taifa. Onyo linatangazwa kwamba jiji litaangamizwa. Kitu kinachoweza kuokoa watu wasiangamie ni kutubu. Lakini badala ya kutubu walijitumainia wenyewe. Wakaamini silaha zao na kuwatumainia wapagani. Nabii anaomboleza kwa ajili ya hali hii. Taifa limekosa utakatifu. Bila Mungu hakuna ushindi. Viongozi wanao wajibu wa kuwaongoza watu wamtegemee Mungu, si kuwapotosha. Nia njema huongozwa na Mungu.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 07/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Julai pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Isaya na 1 Petro. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz