Soma Biblia Kila Siku 09/2025Mfano

Kanisa la Korintho lilikabiliwa na mafundisho ya utamaduni na mapokeo ya Kigiriki. Wagiriki walitenganisha mwili na roho. Hawakuamini juu ya ufufuo wa mwili. Waliona kuwa ufufuo unaihusu roho peke yake na siyo mwili. Walikaza kuwa mwili ni gereza la roho, ambayo inatengana na mwili kwa njia ya kifo. Biblia inafundisha kuwa mwili na roho havitenganishwi milele (unaweza kusoma zaidi juu ya jambo hili katika 1 Kor 15:46-58). Kristo alifufuka kimwili, na katika ufufuo ataifanya miili yetu ifanane na mwili wake wa utukufu.Ataubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake(Flp 3:21).
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 09/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Septemba pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 1 Nyakati na 2 Wakorintho. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz
