Soma Biblia Kila Siku 09/2025Mfano

Jambo linalokuza utoaji wa nafsi, mali, wakati na maisha ni nini? Siri gani iliwafanya Wakorintho kuomba kuchangia kwa ajili ya kuokoa maisha ya Wakristo maskini kule Yerusalemu? Somo linataja mambo matatu: 1) Furaha yao, wakifurahia neema ya Mungu. 2) Umaskini wao, ambao haukuwazuia kutoa bali kuwawezesha kusikia hali ya waumini wenzao. Na 3) ambalo ni la msingi, wamejitoa kwa Bwana. Hivyo maisha yao yote yalitawaliwa na mapenzi ya Mungu. Upendo wao kwa Mungu ulienea kwa watu wake. Jipime.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 09/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Septemba pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 1 Nyakati na 2 Wakorintho. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz
