Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu
na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
kutega sikio lako kwenye hekima
na kuweka moyo wako katika ufahamu,
na kama ukiita busara
na kuita kwa sauti ufahamu,
na kama utaitafuta kama fedha
na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
ndipo utakapoelewa kumcha BWANA
na kupata maarifa ya Mungu.