1
Mit 3:5-6
Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia
Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.
Linganisha
Chunguza Mit 3:5-6
2
Mit 3:7
Usiwe mwenye hekima machoni pako; Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.
Chunguza Mit 3:7
3
Mit 3:9-10
Mheshimu BWANA kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote. Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.
Chunguza Mit 3:9-10
4
Mit 3:3
Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
Chunguza Mit 3:3
5
Mit 3:11-12
Mwanangu, usidharau kuadhibiwa na BWANA, Wala usione ni taabu kurudiwa naye. Kwa kuwa BWANA ampendaye humrudi, Kama vile baba mwanawe ampendezaye.
Chunguza Mit 3:11-12
6
Mit 3:1-2
Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu. Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani.
Chunguza Mit 3:1-2
7
Mit 3:13-15
Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu. Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi. Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye.
Chunguza Mit 3:13-15
8
Mit 3:27
Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda.
Chunguza Mit 3:27
9
Mit 3:19
Kwa hekima BWANA aliiweka misingi ya nchi; Kwa akili zake akazifanya mbingu imara
Chunguza Mit 3:19
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video