1
Waebrania 13:5
Biblia Habari Njema
Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: “Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa.”
Linganisha
Chunguza Waebrania 13:5
2
Waebrania 13:8
Yesu Kristo ni yuleyule jana, leo na milele.
Chunguza Waebrania 13:8
3
Waebrania 13:6
Ndiyo maana tunathubutu kusema: “Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?”
Chunguza Waebrania 13:6
4
Waebrania 13:16
Msisahau kutenda mema na kusaidiana, maana hizi ndizo tambiko zinazompendeza Mungu.
Chunguza Waebrania 13:16
5
Waebrania 13:15
Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu tambiko ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa kwa midomo inayoliungama jina lake.
Chunguza Waebrania 13:15
6
Waebrania 13:4
Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, na haki zake zitekelezwe kwa uaminifu. Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
Chunguza Waebrania 13:4
7
Waebrania 13:2
Msisahau kuwakaribisha wageni; maana kwa kufanya hivyo watu wengine walipata kuwakaribisha malaika bila kujua.
Chunguza Waebrania 13:2
8
Waebrania 13:20-21
Mungu amemfufua katika wafu Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele. Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze matakwa yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina.
Chunguza Waebrania 13:20-21
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video