Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021Mfano

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

SIKU 28 YA 30

Mungu anamzidishia Ayubu maarifa kumhusu yeye. Lengo ni kumwezesha ajue kuwa maswali na changamoto za maisha hazitatuliwi au kujibiwa zote na hekima au ujuzi wa binadamu. Tunachokifahamu ni kile ambacho Mungu ametujalia kutufunulia. Kufahamu hivyo, kunafungua fursa ya kumwamini Mungu: Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni; nawe utanijulisha hekima kwa siri (Zab 51:6). Ujuzi anaoupokea Ayubu ni ufahamu mpya na kuongeza fursa ya kumwamini Mungu atakavyo. Siri ya Mungu i katika Neno lake.

siku 27siku 29

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 1 Wakorintho na Ayubu. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuishukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi tembelea: http://www.somabiblia.or.tz