Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021Mfano

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

SIKU 29 YA 30

Majibu ya Mungu kwa Ayubu yanakusudia kumfundisha kuwa Mungu ni Mwenyezi, hapimiki. Uwezo na ujuzi wa mtu uko chini ya Mungu. Changamoto alizo nazo Ayubu hazizidi wala hazifai kuwekwa katika kapu moja na uweza wa Mungu. Maswali anayoulizwa Ayubu yanathibitisha mwanadamu alivyo na uwezo mdogo juu ya Mungu. Mungu hahitaji majibu. Huu sio mtihani wa kujibiwa bali ni kuvuta unyenyekevu wa mtu kwa Muumba wake. Ndivyo anavyokusudia Mungu akituhoji. Mbele ya Mungu mtu anajipambanua alivyo.

siku 28siku 30

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 1 Wakorintho na Ayubu. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuishukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi tembelea: http://www.somabiblia.or.tz