Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Tafakari Kuhusu HakiMfano

Tafakari Kuhusu Haki

SIKU 23 YA 31

Nimekuwa nakaa na maneno ya Mithali 3:27-28 kwa muda wakati wa Sabato, na vile vile wakati wa kusoma kuhusu umuhimu wa kuheshimu kila mara, Sabato ya Mungu iliyoteuliwa.

Vifungu hivi vinaweza kuchemsha ndani yangu ‘mwito wa wajibu’ ninapokuwa tayari nimechoka ‘kutenda mema’. Kwa mfano, napenda kupika chakula na kukipeleka kwa mtu ambaye amefiwa mda si mrefu, lakini hili limetokea mara chache katika shughuli za huduma ya kanisa. Vifungu hivi vinaweza kuniacha mimi na hisia ya hatia au kujisikia sifanyi kwa kutosheleza.

Hata hivyo, ‘kutenda kwa haki’ vile vile ni pamoja na kutenda vema kwa makusudi kwetu wenyewe. Kitu hutendeka kwetu tunapoheshimu pumziko la Sabato. Walter Brueggemann anaeleza: ‘Sabato sio tu pumziko linaloburudisha. Ni pumziko linalobadilisha.’ Tunaporudi kwenye kazi yetu ya kila siku tunakuwa tuko vizuri zaidi, tumepumzika na tuwasikivu. Tunaweza sana kusema, ‘Napatikana!’

Changamoto: Najiuliza kama unajisikia kuvutwa kuchunguza kwa kina mwaliko wa Mungu wa kuheshimu pumziko la Sabato? Hili linaweza kukubadilisha namna gani na kukufanya uwe unapatikana zaidi kutenda mara moja?

Maombi: Bwana, kwa sababu ya wengine na mimi mwenyewe, nisaidie nikubali na nipende zawadi yako ya Sabato. Hebu kwa wakati ‘matendo’ yangu yatokane na hekalu hili.

siku 22siku 24

Kuhusu Mpango huu

Tafakari Kuhusu Haki

Mfululizo wa tafakari ya kila siku kuhusu haki, ulioandikwa na wanawake kutoka kote katika dunia ya Jeshi la Wokovu. Maswala ya haki ya jamii yako mbele sana ya mawazo yetu siku hizi. Mkusanyo huu wa tafakari kuhusu haki ya jamii umeandikwa na wanawake kutoka kote duniani wenye nia na hamu ya kuwasaidia wengine katika jina la Kristo.

More

Tungependa kumshukuru The Salvation Army International kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://salvationarmy.org