1
Yakobo 1:2-3
Neno: Maandiko Matakatifu 2024
Ndugu zangu, hesabuni kuwa ni furaha tupu mnapopatwa na majaribu mbalimbali, kwa sababu mnajua ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
Linganisha
Chunguza Yakobo 1:2-3
2
Yakobo 1:5
Kama mtu yeyote miongoni mwenu amepungukiwa na hekima, basi amwombe Mungu, yeye awapaye watu wote kwa ukarimu wala hana kinyongo, naye atapewa.
Chunguza Yakobo 1:5
3
Yakobo 1:19
Ndugu zangu wapendwa, fahamuni jambo hili: Kila mtu awe mwepesi wa kusikiliza, lakini asiwe mwepesi wa kusema wala wa kukasirika.
Chunguza Yakobo 1:19
4
Yakobo 1:4
Acheni saburi ikamilishe kazi yake, ili mpate kuwa wakamilifu na watimilifu, bila kupungukiwa chochote.
Chunguza Yakobo 1:4
5
Yakobo 1:22
Basi kuweni watendaji wa Neno, wala msiwe wasikiaji tu, huku mkijidanganya nafsi zenu.
Chunguza Yakobo 1:22
6
Yakobo 1:12
Heri mtu anayevumilia wakati wa majaribu, kwa sababu akiisha kushinda hilo jaribio atapewa taji lile la uzima Mungu alilowaahidia wale wanaompenda.
Chunguza Yakobo 1:12
7
Yakobo 1:17
Kila kitolewacho kilicho chema na kilicho kamili hutoka juu, na hushuka kutoka kwa Baba wa mianga, ambaye kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.
Chunguza Yakobo 1:17
8
Yakobo 1:23-24
Kwa maana kama mtu ni msikiaji tu wa Neno wala hatendi kile linachosema, yeye ni kama mtu ajitazamaye uso wake kwenye kioo na baada ya kujiona alivyo, huenda zake na husahau upesi jinsi alivyo.
Chunguza Yakobo 1:23-24
9
Yakobo 1:27
Dini iliyo safi, isiyo na uchafu, inayokubalika mbele za Mungu, Baba yetu, ndiyo hii: ni kuwasaidia yatima na wajane katika dhiki zao na kujilinda usitiwe madoa na dunia.
Chunguza Yakobo 1:27
10
Yakobo 1:13-14
Mtu anapojaribiwa asiseme, “Ninajaribiwa na Mungu.” Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu wala yeye hamjaribu mtu yeyote. Lakini kila mtu hujaribiwa wakati anapovutwa na kudanganywa na tamaa zake mwenyewe zilizo mbaya.
Chunguza Yakobo 1:13-14
11
Yakobo 1:9
Ndugu asiye na cheo kikubwa yampasa ajivunie hali hiyo maana ametukuzwa.
Chunguza Yakobo 1:9
Nyumbani
Bibilia
Mipango
Video