1
Walawi 26:12
BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA
Nitatembea kati yenu na kuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu.
Linganisha
Chunguza Walawi 26:12
2
Walawi 26:4
nitawanyeshea mvua wakati ufaao, nchi ipate kuzaa mavuno kwa wingi, nayo miti ya mashambani matunda yake.
Chunguza Walawi 26:4
3
Walawi 26:3
“Kama mkifuata masharti yangu na kuzishika amri zangu
Chunguza Walawi 26:3
4
Walawi 26:6
Nitawapeni amani nchini hata muweze kulala bila ya kuogopeshwa na chochote. Nitawaondoa wanyama wakali katika nchi na nchi yenu haitakumbwa na vita.
Chunguza Walawi 26:6
5
Walawi 26:9
Nitawafadhili na kuwajalia mpate watoto wengi na kuongezeka; nami nitaliimarisha agano langu nanyi.
Chunguza Walawi 26:9
6
Walawi 26:13
Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, niliyewatoa nchini Misri ili msiwe watumwa wa Wamisri. Mimi nimevunja nira mliyofungiwa shingoni mwenu na kuwafanya mtembee wima.
Chunguza Walawi 26:13
7
Walawi 26:11
Nitaweka maskani yangu miongoni mwenu, wala sitawaacheni.
Chunguza Walawi 26:11
8
Walawi 26:1
“Msijitengenezee sanamu za miungu ya uongo, msishike sanamu zao za kuchonga wala nguzo wala sanamu za mawe yaliyochongwa nchini mwenu na kuvisujudu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.
Chunguza Walawi 26:1
9
Walawi 26:10
Wakati wa mavuno mtakuwa bado mnakula mazao ya zamani; tena itawalazimu kuondoa yaliyobaki kupata nafasi ya kuhifadhi mavuno mapya.
Chunguza Walawi 26:10
10
Walawi 26:8
Watano wenu watawafukuza adui 100 na 100 wenu watawafukuza adui 10,000. Adui zenu wataangamia mbele yenu kwa upanga.
Chunguza Walawi 26:8
11
Walawi 26:5
Kupura nafaka kutaendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu, na uvunaji zabibu mpaka wakati wa kupanda mbegu. Mtakuwa na chakula tele na kuishi kwa usalama nchini mwenu.
Chunguza Walawi 26:5
12
Walawi 26:7
Mtawafukuza adui zenu na kuwaua kwa upanga.
Chunguza Walawi 26:7
13
Walawi 26:2
Shikeni sabato zangu na kuheshimu mahali pangu patakatifu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.
Chunguza Walawi 26:2
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video