Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ahadi za kila siku ya maisha yakoMfano

Ahadi za kila siku ya maisha yako

SIKU 20 YA 30

Kuruhusu upendo wa Mungu kushinda uchungu wa zamani 


 Mwanzoni mwa ndoa yetu, Dave na   mimi tulikuwa na miaka migumu, na mengi yalikuwa ni kwa sababu nilihitaji Mungu   kuniponya kutokana na uchungu niliokuwa nao wa ule unyanyasaji wa kijinsia,   kihisia na maneno kutoka kwa baba yangu. Kupitia machozi mengi na wakati   mgumu wa kuchagua kusamehe badala ya kulipiza kisasi, Mungu alinipitisha hali   hiyo, na pia alitumia ushuhuda wangu wa kuleta uponyaji kwa maisha ya   wengine.
Wakati Mungu anapo kuponya   kutokana na uchungu wa zamani, sio eti anataka kukusaidia tu, lakini pia   anataka yale uliyopitia yawe njia ambayo wengine wanaweza kupata uponyaji huo   huo.

Hatimaye,   nilifika kiwango ambapo Mungu aliniongoza mimi na Dave kuwahamisha wazazi   wangu hadi St Louis na hata kununua nyumba, ambayo ilikuwa ngumu sana kwangu.   Lakini baba yangu aliniomba msamaha kwa sababu ya yote aliyoyafanya na hata   kumpokea Kristo katika maisha yake.
Nilipata kiwango kipya cha afya ya   kihisia kwa sababu nilimruhusu Mungu aniponye kupitia uwezo wa msamaha na   kumruhusu kutumia marejesho yangu ili kumponya baba yangu.
Sote tunaweza kuumia kwa njia   nyingi. Upweke, kukata tamaa, hofu na ukosefu wa usalama una uwezo wa   kutuumiza kwa undani. Sikuweza kuyapita maumivu kutoka machungu yangu ya kale   mpaka nilipopokea na kuhisi upendo wa Mungu na kumruhusu kugeuza hali zote.

Kabla ya   kupata ushindi juu ya uchungu wako, jifunze kupenda na kusamehe wengine,   unapaswa kuona upendo wa Mungu.
Wakati unaposhughulika na mambo   yako ya kale, kumbuka kwamba Mungu anakupenda sana. Biblia inasema kwamba   sisi ni kamili tu wakati tunapokuwa na uzoefu wa upendo wa Kristo, ambao ni   mkuu sana huwezi kamwe kuuelewa kikamilifu. Unapopokea upendo wake, uponyaji   utaanza moyoni mwako na utafanywa kamili na ukamilifu wa maisha yake

OMBI LA KUANZA SIKU

Bwana, naamini   Unaweza kunisaidia kushinda uchungu na maumivu ya zamani na kutumia uponyaji   wangu kusaidia wengine. Nisaidie kuona upendo wa Kristo na kunifanya   kukamilika kwa utimilifu wote wa maisha yako na nguvu yako.

Andiko

siku 19siku 21

Kuhusu Mpango huu

Ahadi za kila siku ya maisha yako

Mungu ametupa ahadi tele ambazo tunahitaji kutembea ndani yake. Lakini ni muhimu kuzijua, kuziamini ili tuweze kuziona zikidhirika maishani mwetu. Kila siku, kuna ahadi kwa ajili yako. Unapoanza siku yako, pata kufahamu ahadi hizi! 

More

Tunataka kushukuru Joyce Meyer Ministries kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: tv.joycemeyer.org/kiswahili