Soma Biblia Kila Siku 04/2025Mfano

“Mafuta” ya wanyama yaliangaliwa kama sehemu nzuri sana ya sadaka. Yaliwekwa wakfu na Mungu pamoja na damu ya mnyama inayoathiria kifo chake, ili vitumike kwa ajili ya kazi ya upatanisho. Kumbuka Law 1-5 inavyokaza kwamba jambo kuu ni kuoshwa dhambi kwa njia ya kutolewa kwa damu ili tuwe na uhusiano wa kweli na Muumba wetu. Hivyo tunaelewa hukumu kali ya mtu kukataliwa mbali na watu wa Mungu kama akila mafuta au damu. M.28-36 inaonyesha jinsi Mungu anavyowapa wanaomtumikia riziki yao ya kila siku (ni vizuri kuirudia mistari).
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 04/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Aprili pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Walawi, Luka na 2 Petro. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz