Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 04/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 04/2025

SIKU 9 YA 30

“Mikate isiyotiwa chachu” ni mfano wa usafi na uwazi. Kama watu wakienda mbele za Mungu na kufanya ibada bila moyo mweupe, badala ya kupokea baraka walikataliwa mbali na watu wa Mungu. Mtu asidai kwamba ana uhusiano na Mungu kwa njia ya kutoa sadaka, huku akiendelea kung’ang’ania dhambi. Ibada ya kweli kwa Mungu inatakiwa ianzie ndani ya moyo. Zingatia ilivyoandikwa katika 1 Kor 11:27-30:Kila aulaye mkate huo, au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa amejipatia hatia ya mwili na damu ya Bwana. Lakini mtu ajihoji mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe. Maana alaye na kunywa, hula na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kutokuupambanua ule mwili. Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio hawawezi na dhaifu, na watu kadha wa kadha wamelala. Tujihoji kwanza ili tusishiriki Meza ya Bwanaisivyostahili, yaani tusiende mbele za Mungu kwa mioyo ya unafiki na mazoea.

siku 8siku 10

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 04/2025

Soma Biblia Kila Siku 04/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Aprili pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Walawi, Luka na 2 Petro. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz