Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 04/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 04/2025

SIKU 13 YA 30

Jumapili ya leo tunakumbuka siku ya mitende. Hii siku imepewa jina lake kwa sababu wakazi wa Yerusalemu walimpokea Yesu akiwa amepanda mwana-punda kwa mashangilio ya matawi ya mitende kama ishara ya kumpa heshima.Watu wengi wakatandaza mavazi yao njiani, na wengine matawi waliyoyakata mashambani(Mk 11:8). Ingawa watu hawa walionyesha heshima kwa Yesu, siku chache baadaye walipiga kelele kuwa asulubishwe. Kwa nje walionyesha wanampenda, lakini mioyoni mwao walikuwa kinyume naye. Usiwe mnafiki. Ukimpenda Yesu, maanisha hivyo kwa moyo wako wa ndani kwa kweli kabisa.

siku 12siku 14

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 04/2025

Soma Biblia Kila Siku 04/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Aprili pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Walawi, Luka na 2 Petro. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz