Soma Biblia Kila Siku 04/2025Mfano

Nafasi ya Haruni na wanawe haikuwa nyepesi. Walitakiwa kuwawekea watu uzima na mauti, na baraka na laana. Wamtumikie Mungu kwa moyo, akili na mwili wao wote. Hivyo damu ya kondoo wa kuwaweka wakfu ilitiwa kwenye sikio ili lisikie Neno la Mungu, kwenye mkono ili ufanye matendo ya Mungu, na kwenye mguu ili uende katika njia ya Mungu. Kulia ni upande wa heshima. Tena ilibidi wakae siku saba kuandaliwa kipekee. Inatuonyesha kuwa kuitwa kwa kazi ya Mungu si jambo dogo; inatakiwa ukae karibu na Mungu.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 04/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Aprili pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Walawi, Luka na 2 Petro. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz