Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 09/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 09/2025

SIKU 10 YA 30

Inaonekana Wakristo wa Korintho waliuliza kwa nini Paulo hakufika kwao kama walivyotazamia. Jibu ni kwamba katika mabadiliko yote yaliyotukia katika mipango ya safari ya Paulo, kusudi limekuwa moja tu,Kuwahurumia(m.23). Tafakari mfano bora anaoutoa Paulo kwa njia ya maisha yake kwa viongozi wa kanisa. Siye mtawala juu ya waamini nini na wafanye nini, bali nimsaidizi wa furahaya waumini. Furaha hii ni pamoja na uhakika kwamba katika Yesu ahadi zote za Mungu zimekuwa ”Ndiyo”. Rudia tena kusoma na kutafakari m.20:Ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin; Mungu apate kutukuzwa kwa sisi.

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 09/2025

Soma Biblia Kila Siku 09/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Septemba pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 1 Nyakati na 2 Wakorintho. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz

Mipangilio yanayo husiana