Soma Biblia Kila Siku 09/2025Mfano

Agano jipya, ambalo lilifunuliwa na kuanzishwa na Yesu, linaleta matumaini. Mungu sasa anajulikana, anaonekana, anafikika, na anawasiliana nasi kwa njia ya wazi. Yesu Kristo anasema mwenyewe kwamba ndiye njia halisi na ya kweli ya kuwasiliana na Mungu:Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi(Yn 14:6). Mtu yeyote anayemkubali na kumtegemea Yesu Kristo anaondokana na kizuizi kizuiacho wokovu. Kumwamini Yesu Kristo kunatuleta katika nafasi au eneo la kukutana na Mungu uso kwa uso. Tafakari uwezo wa Injili hii kutubadilisha tufanane na Kristo:Sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho(m.18).
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 09/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Septemba pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 1 Nyakati na 2 Wakorintho. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz
