Soma Biblia Kila Siku 09/2025Mfano

Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake(Zab 24:1). Ni vema tukilitambua hili, maana hivyo tutamtolea Mungu wetu kama Mfalme Daudi na watu wake walivyofanya. Tunaona mwitikio kutoka kwa watu katika kumtolea Mungu baada ya Daudi kuonyesha kwa vitendo. Walikubali kwamba vitu vyote ambavyo mwanadamu anaweza kuwa navyo, vyatoka kwa Bwana. Basi, tumrudishie kwa furaha na moyo wa kupenda. Mfalme Daudi pia aliwaombea baraka kwa Mungu. Tuuige mfano wake.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 09/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Septemba pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 1 Nyakati na 2 Wakorintho. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz