Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 09/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 09/2025

SIKU 5 YA 30

Mtu mmoja alisema, “Mafundisho lazima yafanyike kwa mfano”, yaani vitendo. Msemo huo una ukweli kwa somo la leo. Mfalme Daudi alikuwa amekwisha kutoa mali nyingi kwa ujenzi wa hekalu (soma mwenyewe katika 1 Nya 22 kujua zaidi). Hata hivyo tunaona anatoa tena sadaka kubwa. Kielelezo chake kiliwashawishi watu hata watoe sadaka nyingi na kubwa. Makanisani mara nyingi wahubiri huzungumzia kuhusu utoaji wa matoleo, au fungu la kumi. Lakini wanatakiwa kuwa watendaji wa neno hilo walihubirilo, wakionyesha mfano wa utoaji kwa vitendo.

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 09/2025

Soma Biblia Kila Siku 09/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Septemba pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 1 Nyakati na 2 Wakorintho. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz

Mipangilio yanayo husiana